Friday, February 10, 2012

BAADA YA KUVAMIA MASHAMBA SASA WASABATO WAVAMIA SHULE NA KUITEKA YOTE.

                Wanachama wa THISDASO wanaendesha efoti kubwa katika kijiji cha Ngarenanyuki. Mkutano huo unahudumiwa na Ndugu Jerard Nyaonge (mahubiri) Juma Kibona (Kaya na familia pamoja na Usiku Projecta) na Mchungaji Mahemebea (Afya) ilianza February 5/2012 na unatarajiwa kuisha tarehe 18/2/2012.
             Mbinu kadhaa zimeibuliwa kama njia ya kufanikisha mkutano huo ni pamoja na kushiriki kuvuna mashamba ya nyanya na mahidni kwa wanakijiji wa Kijiji cha Ngarenanyuki.
          Njia nyingine ni kufundisha katika shule ya sekondari ya Momela ambapo walimu bila kujijua wamejikuta wakiwaachia vipindi vyote wana THISDASO ambao wamepanga ratiba upya na kutawala shule yote huku wakimchagua Headmaster wa muda (Salim Nyisarya).
            Moja ya mkakati ni kuwataka wanafunzi wote kuhudhuria vipindi vya efoti kama sehemu ya masomo yao. Kwa mkakati huo baadhi ya wanafunzi wamejikuta wakiomba kubatizwa.
kusaidia wenye shida, kujitolea kufundisha, kuvuna mashamba ya wanakijiji hizi ni mbinu ambazo zimefaulu sana.
habari hizi zinapatikana pia    thisdasouniversiotyofarusha.blogspot.com
wawakilishi wa chama cha THISDASO wakiwa wametoka kumpa babu na bibi
zawadi za nguo na vyakula tele tele kutokana na michango ya wanachama.



BAADA YA WASABATO KUVAMIA MASHAMBA SASA WAVAMIA SHULE NA KUPORA.

                      Na Juma Kibona-Mwandishi.
                       Baada ya wale wainjilisti wasabato kukutwa wakivamia mashamba na kufanya kazi ya kusaidia kazi za kuvuna (kama wanavyoonekana pichani) sasa wameongezea mtindo mwingine na kupora akili za wanafunzi wote wa kuanzia kidato cha kwa nza hadi cha nne.
                      Hilo limejitokeza katika shule ya sekondari ya Momela baada ya wana THISDASO kuamua kujitolea kufundisha kila siku za kazi asubuhi hadi mchana kabla ya kuanza mikutano ya jioni ya kila siku. mbinu hiyo imeonesha mafanikio makubwa kwani wanafunzi hao wamejikuta wakihudhuria karibu wote na huku wakitoka bila kusahau kujaza kadi za ubatizo.
                      Bila kujielewa walimu wa shule hiyo wameacha vipindi vyote kwa walimu hawa wasabato. wanafunzi wengi wamegundulika kujaza na kwa dhati kusubiri ubatizo.Athari zilizoipata shule hiyo ni pamoja na ratiba ya shule kupangwa upya kwa kufuata vile wasabato hao wapendavyo. hata hivyo vipindi vyote kwa sasa huanza na maombi kabla ya kuendelea na somo.
                      Wakati huo huo imeonekana kuwa wanachama zaidi wanahitaji vipindi. vijizuu kadhaa hugawiwa kwa wanafunzi kila siku. Head Master wa muda (Salimu Nyisarya) amekaririwa akisema, "Shule hii tutaihubiri na kufundisha hadi kieleweke".

Monday, February 6, 2012

MKUTANO WAPAMBA MOTO


WATU 86 WAUNGUA KWA MOTO NGARENANYUKI NA 7 KUFA.

Na Juma Kibona – Mawasiliano THISDASO UOA.
Katika mkutano wa efoti uliofanyika jana 6/2/2012 hapa Ngarenanyuki-USA River – Arusha, watu 86 (watu wazima wageni tu) walihudhuria na hakika walichomwa na neno la Mungu linaloweza kuchoma kila moyo wa mwanadamu. Ilipofika mwisho wa mkutano watu 7 waliamua kuifia dhambi na kufufuka katika utukufu wa Bwana. Aidha wanakijiji hawa, wamekiri kuwa Yesu anawapenda sana. Frolida anasema, “Nimekuwa nikisumbuka sana ili nipate mme nimekuja kuombewa ili niolewe”. Watu wa Mungu waliomba naye na akafurahi kwamba bila shaka Bwana atafanya muujiza.
Efoti hii inaendesha na kusimamiwa na wanachama wa THISDASO tawi la University of Arusha. Mkutano huu ulianza tarehe 5/2/2012 na utamalizikia tarehe 18/2/2012. Mkutano huu umeambatana na matembezi. Ambapo kila siku asubuhi wanachama hawa hutembelea wanakijiji wote wa Ngarenanyuki.
Leo 7/2/2012, kati ya waliotembelewa na Mzee “Selewani” Silvano ambaye ana miaka 130 kama alivyosema. Mzee huyu anasema, “Nilikuwa na watoto 6, wanne kati yao walikuwa wa kiume na walikwishafariki wote kwa tatizo la UKIMWI, wamebaki 2 wa kike ambapo mmoja hajulikani alipo na mmoja alishaachika tunaye hapa. Sina chakula wala nguo kama mnavyoniona hata jana hatukula”. Wana THISDASO wamepanga kumtembelea na kutoa huduma nyumbani kwa mzee huyu.
Waweza kutembelea pia    thisdasouniversityofarusha.blogspot.com

waliojitoa wakiwa katika darasa la kuchunguza maandiko chini ya Katibu wa THISDASO ndugu Mwizuka Tilunganyila.

Thursday, February 2, 2012

NAWASALIMU KATIKA JINA LA BWANA.
                  Taarifa za hivi karibuni zinasema kuwa asubuhi ya Ijumaa ya tarehe 3/2/2012 vijana wa THISDASO wameondoka kwenda Ngarenanyuki kwenye efoti wakati wengine wakiwa wanaelekea Makwao. Akihojiwa mmoja wa wanachama hao aitwaye Leah Karangi amesema "ni kutokana na kuendea mahitaji kwa wazazi inatulazimu kwenda makwetu" Hata hivyo mjumbe wa programu zote Aunt Masegenya au Mama Mkingira naye alikaririwa akisema "Ninawatakia wanachama wote effort njema" Huku akionesha kutamani kuhudhuria.
                              Vijana wa Kisabato wapatao 85 wanahudhuria mkutano huo, aidha mafundisho ya Neno la Mungu yataongozwa na Mwalimu Nnyaonge, Semina za Afya zitaongozwa na Mchungaji na Mwasitete na Semina za Kaya na Familia zitaongozwa na Mwalimu Kibona kutoka Mpanda. Unatarajiwa kuwa mkutano wenye mafanikio.

Find more music like this on G5 world

Find more music like this on G5 world

habari zote za maisha tukutane kwaticha.blogspot.com