Friday, June 15, 2012


WAVULANA MAARUFU NA WAZURI.
By Mwalimu KIBONA.
Kwanza kabisa asante kwa moyo wako wa kushirikiana nami na kuruhusu majibu yako niyaweke katika blog japo kwa ufupisho tu. Pili nakushauru tu kwamba si wewe wa kwanza kuwa maarufu na hata hivyo mimi sioni kama wewe ni maarufu. Kwa lipi una umaarufu ? Nichokitathmini kwa haraka wewe ni mzuri na unao mvuto kwa mabinti. Unavyokausha kana kwamba bado upo upo unawaumiza wengi na sio vizuri.
Hebu zingatia mambo saba (7) yafuatayo yatakusaidia zaidi ya mno iwapo utayatafakari.
1.     Wewe sio mvulana wa kwanza kuwa maarufu (japo si maaurufu). Alikuwepo akina Eliya, Hanani, na wengineo waliokuwa maarufu katika ujana wao na waliishi Yerusalemu (I Nyakati 8:28), Androniko na Yunia walikuwa vijana maarufu kipindi cha agano jipya (Warumi 16:7).
2.     Walikuwepo Wavulana wazuri kama Sauli (I Samweli 9:2), Daudi ( I Samweli 16:18), Musa (Matendo 7:20), na wengineo wengi.
3.     Unaposoma habari za ndoa za hao wote (wavulana Maarufu na Wazuri hapo juu) wengi wao ndoa zao ziliwasumbua sana, hazikuwa vile Wavulana wengi maarufu kama wewe wanavyotarajia.
4.     Wavulana wote maarufu hupenda kuoa wanawake ambao dunia itasema hakika amepata kitu chenyewe kama yeye mwenyewe alivyo wa juu.
5.     Ili kuunoesha ulimwengu kuwa wameoa wavulana maaurufu hupenda kuoa wasichana walio kama wao kwa elimu, kipato, umaarufu n.k jambo ambalo ni kosa kubwa.
6.     Biblia imesema mke amtii mume (soma Waefeso 5:22-24) Kutiiwa ndio sumu kali inayowavuta wanaume kwa wanawake wa nje ni jambo ambalo likifanywa na mke wa ndani ndoa huwa bora na yenye kunenepesha moyo. Mke anapaswa kumfanya mme kama moja ya watoto wake jambo ambalo haliwezi kutendwa na msichana mnayelingana naye elimu, umri, urefu, kipato n.k. (kivipi – tuwasiliane kwa e mail)
7.     USHAURI – Uzoefu unaonesha kuwa ukitaka kupata mke ambaye atakuwa mke, unatakiwa kutafuta msichana unayemzidi kwa kila kitu yaani kipato, umri, urefu, unene, nguvu, elimu n.k. kwani hayo yatamjengea hisia za kukutii (rejea namba 6 hapo juu) atakuona uko juu yake nawe utapata nafasi ya kuonwa hivyo. Pamoja na ukweli huo ni lazima awe mzuri kwako (anakuvutia). Kwa mfano kama wewe una shahada utatakiwa kuoa mwenye cheti au stashahada.
NB: Tuwasiliane kwa e mail tupange appointment kwa ufafanuzi wa hoja saba hapo juu, maana sio rahisi kuanika kila kitu kwenye blog.

No comments:

Post a Comment